Total Pageviews

Saturday, 22 July 2017

DOWNLOAD NA SIKILIZA WIMBO UITWAO "TUTAPATAJE WOKOVU", WIMBO WA KWAYA NZURI KUTOKA KWAYA YA "MWISENGE ADVENTIST CHOIR"



UNAPENDA MUZIKI MTAMU?........... #Mwisenge_Adventist_Church_Choir wanakuletea wimbo uitwao #Tutapataje_Wokovu.........Ingia na download.

https://gospelmusikcloud.com/track/tutapataje-wokovu/

HISTORIA YA WIMBO-MSIFU MUNGU




#Historia_Ya_Wimbo_Msifu_Mungu*

#PRAISE_GOD_FROM_WHOM_ALL_BLESSING_FLOW_

πŸ‘‰πŸΏ Ni wimbo ambao ulitungwa na kuandikwa na *Bishop Thomas Ken*

πŸ‘‰πŸΏ Katika kitabu cha nyimbo za Kristo kiitwacho, *"The United Methodist Hymnal"*..........wimbo huu upo No. 95.......katika kitabu kidogo cha kiswahili *"Nyimbo Za Kristo"* wimbo huu upo No. 12.

πŸ‘‰πŸΏ Huko Marekani, kuna tarehe maalumu kila mwaka wa tukio liitwalo , *"Thanks Giving"* ambapo nyimbo hutumika na kutoa sadaka maalumu kwa Mungu, wimbo huu pamoja na nyimbo nyingine kama hizi hutumika sana kwa ajili ya Kumsifu na kumshukuru Mungu............

πŸ‘‰πŸΏ Kitaalamu nyimbo hizi za kumsifu Mungu huitwa , *"Doxology"*........ neno hilo limetolewa katika Lugha ya kigiriki likimaanisha *"Glory Saying-Kusema Utukufu"* ........Yaani *"Holy Trinity-Utatu Mtakatifu"*

πŸ‘‰πŸΏ *Bishop, Thomas Ken*, alizaliwa mwaka *1637 na akafa mwaka 1711*

Maisha yake wanasema kuwa alilelewa kama Yatima lakini alitunzwa na dada yake aliyeitwa *Anna* pamoja na shemeji yake aliyeitwa *Izaak Walton*. Walimpeleka katika shule ya wavulana tupu katika chuo cha *Winchester* toka (1651- 1656).......... na baada ya masomo yake alijiunga chuo kikuu cha *Hart Hall, Oxford, Na New College, Oxford ( BA 1661, MA 1664).

πŸ‘‰πŸΏ Baada ya hapo aliapishwa kuwa *kasisi wa Anglican mwaka 1662, akipagwa katika kuhudumu katika parish mbalimbali nchini uingereza...........Pia mwaka (1679-1680) alichaguliwa kuwa chaplain wa *Princess  Mary wa Orange*........

na mwaka (1683-1684) ,alikuwa chaplain wa *Mfalme wa uingereza, _Mfalme Charles II_*........... Lakini pia mwaka (1685) alichaguliwa kuwa *Bishop* wa *Bath na Wells*

πŸ‘‰πŸΏ Wakati wa utawala wa *Mfalme James II*, Alifungwa katika *mnara wa London-Tower of London* kwa kosa la kutokubaliana na maazimio ya mfalme, ila baadaye walimrudisha kazini. Lakini pia wakati wa kuapishwa kwa mfalme mwingine aliyeitwa *Mfalme William III* , Ken alikataa kuapa kumtii na kufanya naye kazi. Kwa hiyo *Thomas Ken* aliacha kazi yake na akaishi maisha yake yote yaliyobakia katika nyumba ya familia yake *Bwana, Weymouth* huko *Wilshire*.

πŸ‘‰πŸΏ Tarehe mahususi ya lini wimbo huu ulitungwa haifahamiki ila mwaka 1674 ndio tarehe ambapo wimbo ulionekana na kuanza kuimbwa katika mikusanyiko ya Wakristo.

*_HISTORIA YA WIMBO NA MAANA YA WIMBO_*

πŸ‘‰πŸΏ Kuna nyimbo mbili ambazo ni *Awake my soul and with the Sun* na mwingine *Glory to thee, my God , This Night*...........Hizi nyimbo mbili ziliekezea hali ya Asubuhi ,Jioni na Usiku wa manane............nyimbo hizo alizipata katika chemba yake aliyokuwa akilala katika *Chuo cha Winchester* ,na alikumbuka kuwa ni vizuri kuelezea uzuri na upendo wa Mungu asubuhi sana, na ukweli wake wakati wa Usiku.

So, wimbo huu wa *Msifu Mungu*, Ken aliutunga kuelezea mandhari ya fikra hizo hizo kusema utukufu wa Mungu ( *Doxology*)

πŸ‘‰πŸΏ Wimbo huu umeimbwa sana kuliko nyimbo zote katika Ibada za Wakristo duniani.

πŸ‘‰πŸΏ Tazama *Zaburi 96: 11-12* na *Zaburi 150:6*
Uone Doxology ya wimbo upoje.

♻♻♻♻♻♻♻♻

*MUNGU AKUBARIKI*

Imeletwa kwenu na mimi mfasili wako *Polite-Trio*

Tukutane Wakati Mwingine🀝